Wanyamazishe Bwana

Wanyamazishe Bwana

Rose Muhando

Альбом: Wanyamazishe Bwana
Длительность: 5:44
Год: 2019
Скачать MP3

Текст песни

Wanyamazishe Bwana
Milele wanyamaze
Wafunge mpito kwa Yesu
Na wakae kimya kimya

Wanyamazishe Bwana
Wanyamaze
Wafunge mpito kwa Yesu
Na wakae kimya kabisa
Wapofushe macho yao
Wasinione wakae mbali nami
Ah wasinione

Kwa kuwa walitangaza msiba juu yangu
Wala hawakutaka ipone nafsi yangu
Wakafanya sherehe kupitia jina langu
Waliona fahari kutangaza mauti yangu

Wakachuma na pesa kupitia jina langu
Hawakuona vibaya kuumiza familia yangu
Walifanya dhihaka kudhihaki watoto wangu
Ah namtuma malaika nyumbani kwao

Atangaze msiba kwenye familia zao
Namtuma Gabrieli malangoni kwao
Atangaze msiba malangoni kwao
Nawafanye matanga maishani mwao

Natangaza msiba kwenye malango yao
Natangaza matanga nyumbani kwao
Yasikome matanga kwenye familia zao
Laana kifo, iwe juu yao

Wala wasiwe salama watoto wao
Mauti iwe fungu lao
Kushindwa uwe mbele yao
Kwa kuwa mimi nimekutumaini

Wanyamazishwe
Watahayarishwe, wafedheishwe
Wahangaike, waaibike
Kwa kuwa mimi nimekutumaini

Wanyamazishe Bwana
Milele wanyamaze
Wafunge mpito kwa Yesu
Na wakae kimya kimya

Wanyamazishe Bwana
Wanyamaze
Wafunge mpito kwa Yesu
Na wakae kimya kabisa

Wapofushe macho yao
Wasinione wakae mbali nami
Ah wasinione
Ah Mikaeli wa vita namtuma kwao
Upeleke mafarakano kwao
Wasielewane waupwa wao

Nasema wagombane wauma wao
Walane watafunane waupwa wao
Wavurugane waupwa wao
Maadui wapigane waupwa wao

Mungu mwenyezi awe adui wao
Wakitazama kulia wamwone Gabrieli
Wakitazama kushoto wamwone Mikaeli
Mbele yangu wamwone Rafaeli

Wafadhaike
Watahayarishwe
Wagonganishwe
Watayarike usiwape nafasi

Wanyamazishe bwana
Milele wanyamaze
Wafunge mpito kwa Yesu
Na wakimyee milele
Wanyamazishe bwana
Wanyamaze
Wafunge mpito kwa Yesu
Na wakae kimya kabisa
Wapofushe macho yao
Wasinione wakae mbali nami
Ah wasinione
Wanyamazishe bwana
Milele wanyamaze
Wafunge mpito kwa Yesu
Na wakimyee milele
Wanyamazishe bwana
Wafunge mpito kwa Yesu
Wapofushe macho yao
Wasinione wakae mbali nami
Ah wasinione